Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2022

MAVUNDE: UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UJENZI WA MABWAWA YA UMWAGILIAJI ITACHOCHEA KUKUA KWA SEKTA YA KILIMO

Picha
  Naibu Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa An thony Mavunde amesema utekelezaji wa miradi ya mabwawa unaoendelea nchini hivi sasa utasaidia sana kukuza sekta ya kilimo nchini Tanzania na kuongeza eneo kubwa zaidi linalofanya kilimo cha umwagiliaji. Naibu Waziri Mavunde ameyasema hayo leo tarehe 12 Novemba, 2022 wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa bwawa la Membe linalojengwa Wilayani Chamwino, Dodoma. "Katika bajeti ya mwaka 2022/2023 Serikali kupitia Tume ya Umwagiliaji imepanga kujenga jumla ya mabwawa 14 nchi nzima, likiwemo bwawa hili la Membe litakalo kuwa na uwezo wa kuhifadhi maji lita Bilioni 12. Pamoja na bwawa hili kutumika katika shughuli za umwagiliaji, pia litawekwa miundombinu ya kusaidia unyweshaji maji mifugo, kupeleka maji ya matumizi ya majumbani kwa vijiji vinavyozunguka na kuwa sehemu ya utalii kwa wananchi mbalimbali, hatua ambayo itaongeza mapato ya Halmashauri ya Chamwino. Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametuongezea bajeti Wizara ya Kilimo ambapo fedha nyingi zimee

MARUBANI NA WAHANDISI WA NDEGE AINA ZOTE KUPATA MAFUNZO TANZANIA,CHUO CH...

Picha
Chuo cha NIT ambacho kilianzishwa rasmi mwaka 1975 kabla ya kubadilishwa muundo na kuwa chuo kikuu miaka ya karibuni, kwa upande wa usafiri wa anga pia kimekuwa kinatoa mafunzo katika uhandisi na ufundi ndege. Ada ya kusomea urubani Pekee ni sh. milioni 70 badala ya sh. milioni 200 zinazotozwa katika vyuo vya nchi za nje. katika ada hiyo, sh. milioni 21 ni gharama za kozi ya urubani kwa masomo ya awali na kiasi kinachobaki ni gharama ya kuruka angani saa 50 wakati wa mafunzo yatakayofanyika katika hatua mbalimbali.

NIT, CHUO KINACHOPIKA WATAALAMU RELI YA SGR

Picha
Serikali kukazania miradi ya kimkakati yawa chachu  Watanzania kuchangamkia  kozi za reli, meli na anga 

MELI YA KITALII ZAANDAM CRUISE SHIP IMETIA NANGA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Picha

WANAZUONI WA CHUO CHA DIPLOMASIA WAJADILI JUU YA SENSA YA WATU NA MAKAZI INAVYOWEZA KUTUMIKA KATIKA UTEKELEZAJI WA DIPLOMASIA YA UCHUMI. TAREHE 8 NOVEMBA 2022

Picha
Desderia Sabuni- Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa Chuo cha Diplomasia akijadili juu ya Sensa ya watu na makazi (2022) inavyoweza kutumika katika Diplomasia ya Uchumi Tanzania.   Seif Ahmad Kushengo Mratibu wa Sensa Kitaifa akitoa maelezo ya awali juu ya Zoezi zima la Sensa livyofanyika kitaifa Balozi Mstaafu Modest Jonathan Mero akijadili Sensa ya Watu na Makazi inavyoweza kutumika katika Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi. Tarehe 8 Novemba 2022 Desderia Sabuni mhadhiri  msaidizi na mkuu wa idara ya Uhusiano wa kimataifa na D iplomasia,mbobezi katika diplomasia ya uchumi  " Sensa inatoa dira ya uvutiaji wa wawekezaji,kiwango cha watu walioko nchini inaweza ikawa chachu ya fursa za uwekezaji nchini katika upatikanaji wa ajira,uwepo wa mitaji na uwepo wa soko." Wanafunzi wa Chuo cha Diplomasia wakifuatilia mjadala wa Sensa ya Watu na Makazi inavyoweza kutumika katika Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi. Symphrosa Chaha Mratibu wa Mjadala wa Sensa ya Watu na Makazi inavy

ASILIMIA 40 YA WATU DUNIANI WANAKABILIWA NA UHABA WA MAJI

Picha
Mtu mmoja kati ya wanne wataishi katika nchi ambako ukosefu wa maji utakuwa ni tatizo sugu na linalojirudia ifikapo mwaka 2050. maji salama na usafi kwa wote ambalo ni lengo namba 6 la SDG’s ni muhimu katika kutimiza malengo mengine, na linachangia katika kupunguza umasikini, kukuza uchumi na kuwa na mifumo bora ya maisha. Hatuwezi kuichukulia amani au rasilimali ya thamani ya maji kimzaha. Kwani kwa hakika maji ni suala la uzima na mauati, miili yetu asilimia 60 ni maji. Miji yetu, viwanda vyetu na kilimo chetu vyote vinayategemea rasilimali hiyo.” Kote duniani hivi sasa zaidi ya watu bilioni mbili hawana fursa ya kupata maji salama na zaidi ya bilioni 4.5 hawana huduma za kutosha za usafi na kujisafi.