Kutoka Kuku 830 Hadi 5,000: Safari ya Mama Shemsa Taraba Kuandika Upya Hadithi ya Ufugaji Zanzibar
Katika kijiji cha Paje Mjogooni, Unguja – Zanzibar, Mama Shemsa John Taraba ameibuka kama mfano bora wa mwanamke mjasiriamali aliyegeuza changamoto kuwa fursa kupitia ufugaji wa kuku wa mayai. Kupitia juhudi zake, ameonyesha kuwa kilimo na ufugaji si kazi ya wanaume pekee, bali ni nyenzo ya kiuchumi kwa kila Mtanzania mwenye maono na dhamira ya kufanikisha ndoto zake. Safari ya Mama Shemsa ilianza kwa kuku 830 pekee, akizalisha tray 36 za mayai kwa siku. Kwa msaada wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kupitia mkopo nafuu na ushauri wa kitaalamu, alijipatia ujuzi na mtaji uliomuwezesha kufanya mageuzi makubwa. Leo hii, anafuga kuku 5,000 wanaozalisha wastani wa tray 145 kwa siku – huku soko likibaki na kiu ya zaidi ya uzalishaji wake. Mafanikio ya Mama Shemsa yameacha alama kubwa kijijini na Zanzibar kwa ujumla: Mahitaji makubwa ya bidhaa – mayai yake yanauzwa kabla hata hayajazalishwa. Ajira kwa jamii – amewaajiri vijana na wanawake wa Paje, na kuongeza k...