Machapisho

Kutoka Kuku 830 Hadi 5,000: Safari ya Mama Shemsa Taraba Kuandika Upya Hadithi ya Ufugaji Zanzibar

Picha
  Katika kijiji cha Paje Mjogooni, Unguja – Zanzibar, Mama Shemsa John Taraba ameibuka kama mfano bora wa mwanamke mjasiriamali aliyegeuza changamoto kuwa fursa kupitia ufugaji wa kuku wa mayai. Kupitia juhudi zake, ameonyesha kuwa kilimo na ufugaji si kazi ya wanaume pekee, bali ni nyenzo ya kiuchumi kwa kila Mtanzania mwenye maono na dhamira ya kufanikisha ndoto zake. Safari ya Mama Shemsa ilianza kwa kuku 830 pekee, akizalisha tray 36 za mayai kwa siku. Kwa msaada wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kupitia mkopo nafuu na ushauri wa kitaalamu, alijipatia ujuzi na mtaji uliomuwezesha kufanya mageuzi makubwa. Leo hii, anafuga kuku 5,000 wanaozalisha wastani wa tray 145 kwa siku – huku soko likibaki na kiu ya zaidi ya uzalishaji wake. Mafanikio ya Mama Shemsa yameacha alama kubwa kijijini na Zanzibar kwa ujumla: Mahitaji makubwa ya bidhaa   – mayai yake yanauzwa kabla hata hayajazalishwa. Ajira kwa jamii   – amewaajiri vijana na wanawake wa Paje, na kuongeza k...

UTEUZI WA WANACHAMA WA CCM WATAKAOGOMBEA NAFASI ZA UBUNGE NA UJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI KWA MAJIMBO NA VITI MAALUM

Picha
TAARIFA KWA UMMA Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinapenda kuwajulisha wanachama wake na umma wa Watanzania kuwa, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) katika kikao chake cha tarehe 23 Agosti, 2025 imefikira na kufanya uteuzi wa mwisho wa majina ya wanachama wanaoomba nafasi za Ubunge na majina ya wanachama wanaoomba nafasi ya Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa majimbo na Viti Maalum. Majina ya walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-   MKOA WA ARUSHA 1. Ndg. Paul Chrisant  MAKONDA Arusha Mjini 2. Dkt. Johannes Lembulung’  LUKUMAY Arumeru Magharibi 3. Ndugu Daniel Awack  TLEMAH Karatu 4. Dkt. Steven Lemomo  KIRUSWA Longido  5. Ndugu Joshua  NASSARI Arumeru Mashariki 6. Ndugu Isack   COPRIAO Monduli  7. Ndugu Yannick Ikayo  NDOINYO Ngorongoro        DAR ES SALAAM 1. Ndugu Haran Nyakisa  SANGA Kigamboni  2. Ndugu Angellah Jasmine  MBELWA    KAIRUKI Kibamba  3. Prof. Alexander Kitila  MKUMBO Ubun...