Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi atembelewa na Madaktari wapya kutoka China wakiongozwa na Balozi mdogo wa China, Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng







 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema ujio wa madaktari bingwa kutoka China ni fursa adhimu kuimarisha sekta ya Afya Zanzibar.
 
Dk. Mwinyi amesema timu ya madaktari bingwa kutoka China imewasili Zanzibar kuongeza nguvu katika sekta ya Afya kwa kutoa wataalamu mbalimbali wakiwemo Madaktari bingwa wa operesheni bila kupasua, magonjwa ya kina mama, magonjwa ya meno, magonjwa ya koo, macho na masikio pamoja na kutoa vifaa vya kisasa.
 
 
Madaktari hao watafanya kazi za kitabibu katika hospitali za Mikoa ya Unguja na Pemba ikiwemo Hospitali ya Mnazi Mmoja, Abdalla Mzee, Chake Chake na Kivunge.
 
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipotembelewa Ikulu Zanzibar na Madaktari wapya kutoka China 
 
Ujumbe huo wa Madaktari umeongozwa na Balozi mdogo wa China, Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng
 
 
📅 08 Februari 2023
 
📍 Ikulu ,Zanzibar.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MJI WA KILWA KISIWANI ULIVYOBEBA HISTORIA YA MATAIFA MBALIMBALI

RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA MAKAMU WA RAIS WA KAMPUNI YA KIMATAIFA YA PHILIP MORRIS GREGOIRE VERDEAUX IKULU CHAMWINO MKOANI DODOMA