MAPITIO YA SERA NA MITAALA YANAANGAZIA PIA TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA-WAZIRI MKENDA
Na Mathias Canal, WEST-Morogoro Serikali imesema kuwa inaendelea kufanya mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 na mabadiliko ya mitaala ili kuongeza ubora wa elimu na mafunzo. Katika Mapitio hayo ya mitaala na sera pia yanaangazia kwa karibu Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima ili wakati utatuzi wa changamoto ukiendelea serikali kuangalia nini kifanyike ili kuboresha elimu ujuzi kwa wanafunzi ikiwemo watu wazima. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Prof Adolf Mkenda ameyasema hayo leo tarehe 9 Septemba 2022 wakati wa hafla fupi ya ufungaji wa mafunzo ya Baraza la Usimamizi wa Taasisi ya elimu ya watu wazima (TEWW) Kampasi ya Morogoro. Prof Mkenda amesema kuwa Taasisi hiyo inapaswa kushiriki kikamilifu katika utoaji wa maoni ikiwa ni pamoja na kushirikisha kwa karibu wadau wengine kutoa maoni namna ya kuboresha taasisi hiyo hususani katika maeneo ya ujuzi. Pia, Prof Mkenda amesema kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Tek...